Sunday, July 9, 2017

Umezaliwa kushinda sio kushindwa


Kila wakati unapotoka kwenye usingizi tambua kwamba umezaliwa kushinda na sio kushindwa, mungu wakati anakuleta dunian alikuandaa uje kushinda na kuja kuwa mtu mkubwa sana. Umeletwa ili utimize kusudi la mungu juu ya utukufu wake juu yako kwa jinsi alivyokuumba na kukupa maarifa makubwa sana ambayo kama utayatumia basi utashinda daima.
Mungu amekupa kila aina ya uwezo ndani yako unaokuwezesha wewe kushinda na kukufanya uwe mkubwa kila siku. usikubali kitu au mtu yoyote kukutoa kwenye kusudi la maisha yako ya ushindi, pambana bila kuchoka changamoto njia ni hali ya kawaida na ndizo zitakazo kufanya uwe mkubwa kama utazikabili kweli.
Usijisikie unyonge wala kujiona huna thamani pale unapopitia magumu na kudhani mungu amekuleta ili uteseke hapana, kusudi la kuja kwako hapa duniani ni kushinda na kuwa mkubwa kila siku.
Haijalishi udogo wa elimu uliyo nayo, udogo wa mtaji, au udogo wa cheo ulicho nacho. kumbuka umezaliwa kushinda sio kushindwa. ndio maana mungu anakutaarifu juu ya kupambana na shetani ambaye kama hutakuwa imara unawez ukashindwa.
You were born orignal don’t die a copy – Jumaa saidi
Tambua kwamba umezaliwa ukiwa halisi jitahidi usife ukiwa kopi. uwezo uliyoko ndani yako ni mkubwa sana hivyo pambana kila siku , wewe ni mshindi na ni mkubwa sana.
Mungu anakuona, anakujua ndani nje hawezi kukuacha uteseke bali anachotaka mungu ni wewe kupambana bila kuchoka kwa ajili ya kusherekea ushindi wako. Umezaliwa kushinda sio kushindwa.
Usijilinganishe na wengine kwa jinsi vile walivyo navyo , tambua wale unajilinganisha nao kuna wakati walikuwa kama wewe ila wao waliamua kupambana kila siku bila kuchoka na kuupata ukubwa walio nao leo.
Jitahidi kupambana leo kesho tushuudie ukubwa wako.

JE UMEFANIKIWA KUJIUNGA NDANI YA MTANDAO HUU WA MAARIFAPROFITS TANZANIA?
Ukijiunga ndani ya mtandao huu wa Maarifaprofits Tanzania. utaweza kupata vitabu vya maarifa, Biashara na kilimo bure pamoja na makala za mafundisho zitakazo kuwa zimeandaliwa kwa ajili yako.
Kama bado hujajiunga basi unaweza kujiunga hapa kwenye hii linki  JIUNGE NA MTANDAO HUU
Je unafahamu hatua 6 muhimu za mafanikio? ambazo kama ungezijua na kuzitumia ungepata mafanikio yako kwa haraka zaidi na wakati sahihi  Bonyeza maandishi haya kupata kitabu

0 comments: