Sunday, July 9, 2017

USHAURI: umeanzisha biashara lakini hupati wateja




Karibu sana rafiki yangu:
Habari za leo mpenzi  msomaji wa makala ndani ya mtandao wako wa mpekuziforum, ni siku nyengine njema ambayo mungu ametukutanisha siku ya leo kwa ajili ya kutenda mema. Ikumbukwe mbali na kuhainga na maswala ya kidunia dhumuni kubwa ambalo mungu amelileta kwetu ni suala la mimi na wewe kufanya ibada pamoja na kuutukuza utukufu wake kupitia sisi na si vingine.
Rafiki yangu kabla ya kuendelea mbele nadhani unakumbuka kwamba nimeazimia kukwambia ukweli kwenye kila kitu ambacho unakifanya ili uweze kukihitimisha vizuri.
Mara kwa mara nimekuwa nikipokea swali kutoka kwa baadhi ya wanachama wa mtandao huu wa maarifaprofits Tanzania , ya kwamba wameanzisha biashara au wewe umeanzisha biashara lakini wateja hawaji kwako kununua hicho unachouza.
Hili ni swali ambalo huenda linawasumbua sana watu kwenye biashara zao na ndio imekuwa sababu ya wafanyabiashara wengi kukimbilia kwa waganga wa kienyeji kudhani kwamba wamerogwa.
Hakuna mtu anaeweza kukuroga kwenye biashara yako ila ni wewe mwenyewe.
Rafiki yangu Falsafa ama dhana ya biashara ni pan asana na ni ngumu sana huo ndio ukweli na ndio maana kila wakati nakwambia kwamba mafanikio ni safari ndefu sana inayohitaji kujitoa zaidi.
Biashara kuifanya kwenye makaratasi ni rahisi sana lakini kuifanya kwenye vitendo ni ngumu sana,  sio kama nakutisha ama nakukatisha tama ila napenda utambue kwamba huo ndio ukweli. Sitatumia muda wangu kuanza kukukatisha tamaa ila nitatumia muda wangu kukusaidia kwenye kila hali.
Rafiki yangu kuna maswali matatu muhimu ukiweza kuyajibu kwa ufasaha utaweza kutambua ni kwanini wateja wahaji kwenye biashara yako, usikimbilie kumtafuta mchawi, mchawi wa kwanza ni wewe mwenyewe.
Kwenye mada zitakazofata nitakuelezea kwanini nazidi kukwambia kwamba wewe ndio mchawi mkuu kwenye biashara yako.
Chunguza maswali haya kwa makini:
Je hiyo biashara unayofanya au unayotaka kuifanya inahitajika kwenye hilo eneo?
Kabla ya kuanza kufanya biashara jiulize hilo swali je biashara yako inahitajika hapo ulipo, maana ukienda kuianzisha mahali ambapo haitajiki natumbua unajisumbua hakuna mteja atakaye kuja kwako.
Utakuta mtu mahali watu wanahitaji huduma ya maji yeye anakwenda kuanzisha biashara ya saloon, huko ni kufeli kuliko wazi ambapo haitaji kwenda kwa mganga wa kienyeji ili kulijua hilo , kinachoitajika ni wewe kwenda sambamba na hitaji la watu husika.
Kabla kuanzisha biashara yako fanya utafiti wa vitu gani watu wanahitaji  , ukishavijua basi vifanyie kazi.
Wateja wanao uwezo wa kulipia gharama za huduma unayotaka kutoa ama unayotoa?
Swali la pili muhimu sana na hapa ndipo palipo na  mtego ambapo wengi umewashinda kuutegua, natambua lengo la kufanya biashara ni kupata faida lakini sio kigezo cha kumfanya Yule muhitaji kushindwa kulipia gharama.
Haya yote yanatokea na kwasababu ya watu kuingia kwenye biashara kwa matakwa ya watu na sio maamuzi yao, lipo wimbi huko ama huku mtaani ambalo kila siku linawasomba vijana kwa kutokuelewa dhana vizuri ya biashara.
Utakuta vijana wapo kwenye vijiwe wakiambiana uongo eti ukifanya biashara Fulani inakulipa  na ndio imekuwa sababu ya watu kufanya biashara zisizo sahihi mahali husika. Kama kweli unataka kufanya biashara zingatia maswali haya matatu.
Rafiki yangu sababu moja wapo inayowafukuza wateja kwenye biashara yako ni ukubwa wa bei kwenye bidhaa ama huduma unazotoa, weka bei ambazo watu wataweza kulipia.
Chukua mfano wa china baada ya kuona japani wanatengeneza simu nzuri na bora lakini watu wengi hawana uwezo wa kuzinunua kwa sababu ya bei yake kuwa kumbwa ndipo mchina akaja na simu zake za bei ambayo kila mtu anaweza kulipia. Na huenda hata simu unayotumia wewe ni ya kichina.
Jitahidi rafiki yangu kuweka bei ambayo mteja ataweza kulipia.
Je ina ubora kiasi cha kujitangaza yenyewe?
Ubora kwenye biashara ni kitu cha msingi  sana  na ndio huitangaza biashara yako bila ya wewe mwenyewe kujua. Mteja anapokuja kununua bidhaa kutoka kwako ikawa na ubora basi atakusaidia kuitangaza kwa wengine na itakuwa sababu ya wateja kuja kwako kununua mahitaji yao.
Katika nchi nyingi za ulaya hawatumii simu za mchina  unajua kwanini? Ni kwasababu ya ubora wake uko chini sana , hivyo rafiki yangu jitahidi kutoa huduma bora kwa wateja wako kila siku.
Nadhani mapaka hapa nitakuwa nimejibu swali hili kwa mtindo wa maswali, nakuomba usiangaike kwa waganga angaika na maswali haya na uyapatie majibu ya kina ili uweze kuendesha biashara yako vizuri.
Kama bado unahitaji ufafanuzi zaidi usijali , najua uwelewa wetu uko tofauti sana kwani hata watoto mapacha wana D.N.A tofauti, hivyo unaweza kutuma maswali au maoni kwenye email hii maarifaprofits@gmail.com  nitakujibu kwa kadri uwezo alionipa mungu.
Ofa ya kitabu cha HATUA 6 MUHIMU ZA MAFANIKIO imebaki kwa watu wachache sana hivyo kama hujapata nakala yako unaweza kukuipata sasa. Bonyeza linki hapo chini ili uweze kukipata na uweze kukisoma kwenye simu, Pc na hata Tablates.

0 comments: